21. Watu walitangaze jina la BWANA katika Sayuni,Na sifa zake katika Yerusalemu,
22. Pindi mataifa watapokusanyika pamoja,Falme nazo ili kumtumikia BWANA.
23. Amezipunguza nguvu zangu njiani;Amezifupisha siku zangu.
24. Nitasema, Ee Mungu wangu, usiniondoe katikati ya siku zangu;Miaka yako ni tangu kizazi hata kizazi.
25. Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi,Na mbingu ni kazi ya mikono yako.
26. Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumuNaam, hizi zitachakaa kama nguo;Na kama mavazi utazibadilisha,Nazo zitabadilika.
27. Lakini Wewe U Yeye yule;Na miaka yako haitakoma.