Yoe. 3:19-21 Swahili Union Version (SUV)

19. Misri itakuwa ukiwa, na Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya dhuluma waliowatenda wana wa Yuda; kwa sababu wamemwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.

20. Bali Yuda atadumu milele, na Yerusalemu tangu kizazi hata kizazi.

21. Nami nitaitakasa damu yao ambayo sijaitakasa; kwa maana BWANA ndiye akaaye Sayuni.

Yoe. 3