Yoe. 2:15-17 Swahili Union Version (SUV)

15. Pigeni tarumbeta katika Sayuni,Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu;

16. Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko,Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto,Na hao wanyonyao maziwa;Bwana arusi na atoke chumbani mwake,Na bibi arusi katika hema yake.

17. Hao makuhani, wahudumu wa BWANA, na walieKati ya patakatifu na madhabahu,Na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee BWANA,Wala usiutoe urithi wako upate aibu,Hata mataifa watawale juu yao;Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao?

Yoe. 2