Yoe. 1:17-19 Swahili Union Version (SUV)

17. Mbegu zinaoza chini ya udongo wake; ghala zimeachwa ukiwa; mabanda yamevunjika; kwa maana nafaka imekauka.

18. Jinsi wanyama wanavyougua! Makundi ya ng’ombe yamefadhaika, kwa sababu hawana malisho; naam, makundi ya kondoo yamepata mateso.

19. Ee BWANA, nakulilia wewe;Kwa maana moto umeyala malisho ya nyikani,Na miali ya moto imeteketeza miti yote ya mashamba.

Yoe. 1