57. Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
58. Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
59. Basi wakaokota mawe ili wamtupie; lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni.