27. Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako.
28. Basi Yesu akapaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, Mimi mnanijua, na huko nitokako mnakujua; wala sikuja kwa nafsi yangu; ila yeye aliyenipeleka ni wa kweli, msiyemjua ninyi.
29. Mimi namjua, kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.
30. Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.