Yn. 3:33-36 Swahili Union Version (SUV)

33. Yeye aliyeukubali ushuhuda wake ametia muhuri ya kwamba Mungu ni kweli.

34. Kwa kuwa yeye aliyetumwa na Mungu huyanena maneno ya Mungu; kwa sababu hamtoi Roho kwa kipimo.

35. Baba ampenda Mwana, naye amempa vyote mkononi mwake.

36. Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.

Yn. 3