1. Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
2. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
3. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.
4. Nami niendako mwaijua njia.
5. Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?