Yer. 50:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Neno hili ndilo alilosema BWANA, katika habari za Babeli, na katika habari za Wakaldayo, kwa kinywa cha Yeremia, nabii.

2. Tangazeni katika mataifa,Mkahubiri na kutweka bendera;Hubirini, msifiche, semeni,Babeli umetwaliwa!Beli amefedheheka;Merodaki amefadhaika;Sanamu zake zimeaibishwa,Vinyago vyake vimefadhaika.

3. Maana toka kaskazini taifa linakuja juu yake, litakaloifanya nchi yake kuwa ukiwa; wala hapana mtu atakayekaa humo; wamekimbia, wamekwenda zao, mwanadamu na mnyama pia.

Yer. 50