Yer. 49:23-26 Swahili Union Version (SUV)

23. Habari za Dameski.Hamathi umetahayarika, na Arpadi pia;Maana wamesikia habari mbaya;Wameyeyuka kabisa;Huzuni iko baharini, haiwezi kutulia.

24. Dameski umedhoofika;Umejigeuza kukimbia; tetemko limeushika;Dhiki na huzuni zimeupata,Kama za mwanamke katika utungu wake.

25. Imekuwaje mji wa sifa haukuachwa, mji wa furaha yangu?

26. Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika njia kuu zake, na watu wote wa vita watanyamazishwa katika siku hiyo, asema BWANA wa majeshi.

Yer. 49