1. Neno la BWANA likanijia, kusema,
2. Enenda ukalie masikioni mwa Yerusalemu, ukisema, BWANA asema hivi,Nakukumbuka, hisani ya ujana wako,upendo wa wakati wa uposo wako;Jinsi ulivyonifuata huko jangwani,katika nchi isiyopandwa mbegu.
3. Israeli walikuwa utakatifu kwa BWANA;malimbuko ya uzao wake;Wote watakaomla watakuwa na hatia;uovu utawajilia; asema BWANA.
4. Lisikieni neno la BWANA, ninyi nyumba ya Yakobo, na ninyi, jamaa zote za nyumba ya Israeli.
5. BWANA asema hivi, Baba zenu waliona dhuluma gani kwangu, hata wakafarakana nami, wakafuata ubatili, nao wakawa ubatili?
6. Wala hawakusema, Yuko wapi BWANA, aliyetutoa katika nchi ya Misri; akatuongoza jangwani, katika nchi ya ukame na mashimo, katika nchi ya kiu na ya kivuli cha mauti, katika nchi ambayo ndani yake hapiti mtu, wala haikukaliwa na watu?