Yer. 14:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Neno la BWANA lililomjia Yeremia, katika habari ya ukosefu wa mvua.

2. Yuda huomboleza,Na malango yake yamelegea;Wameketi chini wamevaa kaniki;Na kilio cha Yerusalemu kimepaa juu.

3. Na wakuu wao huwatuma watoto wao kwenye maji;Nao hufika visimani wasione maji;Hurudi, na vyombo vyao ni vitupu;Wametahayarika na kufadhaika,Na kuvifunika vichwa vyao.

Yer. 14