Yer. 13:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. BWANA akaniambia hivi, Enenda, ukajinunulie mshipi wa kitani, ukajivike viuno, wala usiutie majini.

2. Basi nikanunua mshipi sawasawa na neno la BWANA, nikajivika viunoni.

3. Nalo neno la BWANA likanijia mara ya pili, kusema,

4. Twaa mshipi ule ulioununua, ulio viunoni mwako, kisha ondoka, enenda mpaka mto Frati, ukaufiche huko katika pango la jabali.

5. Basi nikaenda, nikauficha karibu na mto Frati, kama BWANA alivyoniamuru.

Yer. 13