Yak. 2:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.

14. Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa?

15. Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki,

16. na mtu wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini?

Yak. 2