13. Mashavu yake ni kama matuta ya rihani,Ambayo hufanyizwa manukato;Midomo yake ni kama nyinyoro,Inadondoza matone ya manemane;
14. Mikono yake ni kama mianzi ya dhahabu,lliyopambwa kwa zabarajadi;Kiwiliwili chake kama kazi ya pembe,Iliyonakishiwa kwa yakuti samawi;
15. Miguu yake ni kama nguzo za marimari,Zilizowekwa juu ya misingi ya dhahabu;Sura yake ni kama Lebanoni,Ni bora mfano wa mierezi;