Wim. 1:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Mpendwa wangu ni kama mfuko wa manemaneUkilazwa usiku maziwani mwangu.

14. Mpendwa wangu ni kama kishada cha hina,Katika mizabibu huko Engedi.

15. Tazama, u mzuri, mpenzi wangu,U mzuri, macho yako ni kama ya hua.

16. Tazama, u mzuri, mpendwa wangu,Wapendeza, na kitanda chetu ni majani;

Wim. 1