Rum. 4:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Kama vile Daudi aunenavyo uheri wake mtu yule ambaye Mungu amhesabia kuwa na haki pasipo matendo,

7. Heri waliosamehewa makosa yao,Na waliositiriwa dhambi zao.

8. Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi.

9. Basi je! Uheri huo ni kwa hao waliotahiriwa, au kwa hao pia wasiotahiriwa? Kwa kuwa twanena ya kwamba kwake Ibrahimu imani yake ilihesabiwa kuwa ni haki.

10. Alihesabiwaje basi? Alipokwisha kutahiriwa, au kabla hajatahiriwa? Si baada ya kutahiriwa, bali kabla ya kutahiriwa.

Rum. 4