Rum. 3:9-14 Swahili Union Version (SUV)

9. Ni nini basi? Tu bora kuliko wengine? La! Hata kidogo. Kwa maana tumekwisha kuwashitaki Wayahudi na Wayunani ya kwamba pia wamekuwa chini ya dhambi;

10. kama ilivyoandikwa, ya kwamba,Hakuna mwenye haki hata mmoja.

11. Hakuna afahamuye;Hakuna amtafutaye Mungu.

12. Wote wamepotoka, wameoza wote pia;Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.

13. Koo lao ni kaburi wazi,Kwa ndimi zao wametumia hila.Sumu ya fira i chini ya midomo yao.

14. Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.

Rum. 3