12. Wote wamepotoka, wameoza wote pia;Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.
13. Koo lao ni kaburi wazi,Kwa ndimi zao wametumia hila.Sumu ya fira i chini ya midomo yao.
14. Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
15. Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
16. Uharibifu na mashaka yamo njiani mwao.
17. Wala njia ya amani hawakuijua.
18. Kumcha Mungu hakupo machoni pao.
19. Basi twajua ya kuwa mambo yote inenayo torati huyanena kwa hao walio chini ya torati, ili kila kinywa kifumbwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu;