10. kama ilivyoandikwa, ya kwamba,Hakuna mwenye haki hata mmoja.
11. Hakuna afahamuye;Hakuna amtafutaye Mungu.
12. Wote wamepotoka, wameoza wote pia;Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.
13. Koo lao ni kaburi wazi,Kwa ndimi zao wametumia hila.Sumu ya fira i chini ya midomo yao.
14. Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
15. Miguu yao ina mbio kumwaga damu.