Rum. 15:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wao wasio na nguvu, wala haitupasi kujipendeza wenyewe.

2. Kila mtu miongoni mwetu na ampendeze jirani yake, apate wema, akajengwe.

3. Kwa maana Kristo naye hakujipendeza mwenyewe; bali kama ilivyoandikwa, Malaumu yao waliokulaumu wewe yalinipata mimi.

Rum. 15