Rum. 14:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.

2. Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.

3. Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali.

4. Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.

Rum. 14