1. Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.
2. Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.
3. Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali.
4. Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.