Omb. 4:20-22 Swahili Union Version (SUV)

20. Pumzi ya mianzi ya pua zetu, masihi wa BWANA,Alikamatwa katika marima yao;Ambaye kwa habari zake tulisema,Chini ya kivuli chake tutakaa kati ya mataifa.

21. Furahi, ushangilie, Ee binti Edomu,Ukaaye katika nchi ya Usi;Hata kwako kikombe kitapita,Utalewa, na kujifanya uchi.

22. Uovu wako umetimia, Ee binti Sayuni;Hatakuhamisha tena;Atapatiliza uovu wako, Ee binti Edomu;Atazivumbua dhambi zako.

Omb. 4