15. Watu waliwapigia kelele, Ondokeni, Uchafu,Ondokeni, ondokeni, msiguse;Walipokimbia na kutanga-tanga, watu walisema kati ya mataifa,Hawatakaa hapa tena.
16. Hasira ya BWANA imewatenga,Yeye hatawaangalia tena;Hawakujali nafsi za wale makuhani,Hawakuwaheshimu wazee wao.
17. Macho yetu yamechokaKwa kuutazamia bure msaada wetu;Katika kungoja kwetu tumengojea taifaLisiloweza kutuokoa.
18. Wanatuvizia hatua zetu,Hata hatuwezi kwenda katika njia zetu;Mwisho wetu umekaribia, siku zetu zimetimia;Maana mwisho wetu umefika.