8. BWANA amekusudia kuuharibuUkuta wa binti Sayuni;Ameinyosha hiyo kamba,Hakuuzuia mkono wake usiangamize;Bali amefanya boma na ukuta kuomboleza;Zote pamoja hudhoofika.
9. Malango yake yamezama katika nchi;Ameyaharibu makomeo yake na kuyavunja;Mfalme wake na wakuu wake wanakaaKati ya mataifa wasio na sheria;Naam, manabii wake hawapati maonoYatokayo kwa BWANA.
10. Wazee wa binti Sayuni huketi chini,Hunyamaza kimya;Wametupa mavumbi juu ya vichwa vyao,Wamejivika viunoni nguo za magunia;Wanawali wa Yerusalemu huinama vichwa vyaoKuielekea nchi.
11. Macho yangu yamechoka kwa machozi,Mtima wangu umetaabika;Ini langu linamiminwa juu ya nchiKwa uharibifu wa binti ya watu wangu;Kwa sababu watoto wachanga na wanyonyao,Huzimia katika mitaa ya mji.