12. Wao huwauliza mama zao,Zi wapi nafaka na divai?Hapo wazimiapo kama waliojeruhiwaKatika mitaa ya mji,Hapo walipomiminika nafsi zaoVifuani mwa mama zao.
13. Nikushuhudie nini? Nikufananishe na nini,Ee Binti Yerusalemu?Nikusawazishe na nini, nipate kukufariji,Ee bikira binti Sayuni?Kwa maana uvunjifu wako ni mkuu kama bahari,Ni nani awezaye kukuponya?
14. Manabii wako wameona maono kwa ajili yakoYa ubatili na upumbavuWala hawakufunua uovu wako,Wapate kurudisha kufungwa kwako;Bali wameona mabashiri ya ubatili kwa ajili yakoNa sababu za kuhamishwa.
15. Hao watu wote wapitaoHukupigia makofi;Humzomea binti Yerusalemu,Na kutikisa vichwa vyao;Je! Mji huu ndio ulioitwa, Ukamilifu wa uzuri,Furaha ya dunia yote?
16. Juu yako adui zako woteWamepanua vinywa vyao;Huzomea, husaga meno yao,Husema, Tumemmeza;Hakika siku hii ndiyo tuliyoitazamia;Tumeipata, tumeiona.
17. BWANA ameyatenda aliyoyakusudia; amelitimiza neno lake,Aliloliamuru siku za kale;Ameangusha hata chini,Wala hakuona huruma;Naye amemfurahisha adui juu yako,Ameitukuza pembe ya watesi wako.
18. Mioyo yao ilimlilia Bwana;Ee ukuta wa binti Sayuni!Machozi na yachuruzike kama mtoMchana na usiku;Usijipatie kupumzika;Mboni ya jicho lako isikome.