2. Hulia sana wakati wa usiku,Na machozi yake yapo mashavuni;Miongoni mwa wote waliompendaHakuna hata mmoja amfarijiye;Rafiki zake wote wamemtenda hila,Wamekuwa adui zake.
3. Yuda amehamishwa kwa sababu ya kuonewa,Na kwa sababu ya utumwa mkuu;Anakaa kati ya makafiri,Haoni raha iwayo yote;Wote waliomfuata wamempataKatika dhiki yake.
4. Njia za Sayuni zaomboleza,Kwa kuwa hakuna ajaye kwa sikukuu;Malango yake yote yamekuwa ukiwa,Makuhani wake hupiga kite;Wanawali wake wanahuzunika;Na yeye mwenyewe huona uchungu.