Mwa. 28:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Esau akaona ya kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padan-aramu, ili ajitwalie mke huko, na katika kumbariki akamwagiza, akasema, Usitwae mke wa binti za Kanaani,

7. na ya kuwa Yakobo amewatii babaye na mamaye, akaenda Padan-aramu.

8. Esau akaona ya kuwa binti za Kanaani hawakumpendeza Isaka, baba yake.

9. Basi Esau akaenda kwa Ishmaeli akamtwaa Mahalathi, binti Ishmaeli mwana wa Ibrahimu, ndugu wa Nebayothi, kuwa mkewe pamoja na wakeze aliokuwa nao.

10. Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani.

Mwa. 28