14. Akaenda, akawatwaa, akamletea mamaye. Mamaye akafanya chakula kitamu namna ile aliyopenda babaye.
15. Kisha Rebeka akatwaa mavazi mazuri ya Esau mwanawe mkubwa, aliyokuwa nayo nyumbani, akamvika Yakobo mwanawe mdogo.
16. Na ngozi za wana-mbuzi akamvika mikononi, na katika ulaini wa shingo yake.
17. Naye akampa Yakobo mwanawe mikononi mwake hicho chakula kitamu, na mkate alioufanya.