Mwa. 26:16-18 Swahili Union Version (SUV)

16. Abimeleki akamwambia Isaka, Utoke kwetu, maana wewe una nguvu sana kuliko sisi.

17. Basi Isaka akatoka huko akapiga kambi katika bonde la Gerari, akakaa huko.

18. Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.

Mwa. 26