Mwa. 21:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.

14. Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.

15. Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.

16. Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.

17. Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.

Mwa. 21