1. Akapanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao.
2. Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
3. Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.