Mt. 7:26-29 Swahili Union Version (SUV)

26. Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27. mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

28. Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake;

29. kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi wao.

Mt. 7