Mt. 6:31-34 Swahili Union Version (SUV)

31. Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32. Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33. Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

34. Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.

Mt. 6