8. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,
9. akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.
10. Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
11. Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.
12. Basi Yesu aliposikia ya kwamba Yohana amefungwa, alikwenda zake mpaka Galilaya;
13. akatoka Nazareti, akaja akakaa Kapernaumu, mji ulioko pwani, mipakani mwa Zabuloni na Naftali;
14. ili litimie neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema,
15. Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali,Njia ya bahari, ng’ambo ya Yordani,Galilaya ya mataifa,