Mt. 26:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Wakati ule wakuu wa makuhani, na wazee wa watu, wakakusanyika katika behewa ya Kuhani Mkuu, jina lake Kayafa;

4. wakafanya shauri pamoja, ili wamkamate Yesu kwa hila na kumwua.

5. Lakini wakasema, Isiwe wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu.

6. Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,

7. mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya thamani kubwa alimkaribia akaimimina kichwani pake alipoketi chakulani.

Mt. 26