Mt. 26:25-30 Swahili Union Version (SUV)

25. Yuda, yule mwenye kumsaliti, akajibu, akasema, Ni mimi, Rabi? Akamwambia, Wewe umesema.

26. Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu

27. Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki;

28. kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

29. Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.

30. Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni.

Mt. 26