16. Mara yule aliyepokea talanta tano akaenda, akafanya biashara nazo, akachuma faida talanta nyingine tano.
17. Vile vile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida.
18. Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake.
19. Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.