Mt. 24:39-44 Swahili Union Version (SUV)

39. wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

40. Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;

41. wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.

42. Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu.

43. Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.

44. Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

Mt. 24