39. wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
40. Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;
41. wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.
42. Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu.
43. Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
44. Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.