Mt. 22:3-10 Swahili Union Version (SUV)

3. Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.

4. Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.

5. Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;

6. nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.

7. Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.

8. Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.

9. Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.

10. Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.

Mt. 22