2. Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.
3. Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.
4. Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.
5. Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;
6. nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.