Mt. 21:2-6 Swahili Union Version (SUV)

2. Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana-punda pamoja naye; wafungueni mniletee.

3. Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.

4. Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,

5. Mwambieni binti SayuniTazama, mfalme wako anakuja kwako,Mpole, naye amepanda punda,Na mwana-punda, mtoto wa punda.

6. Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,

Mt. 21