1. Hata walipokaribia Yerusalemu, na kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi wawili akiwaambia,
2. Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana-punda pamoja naye; wafungueni mniletee.
3. Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.
4. Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,
5. Mwambieni binti SayuniTazama, mfalme wako anakuja kwako,Mpole, naye amepanda punda,Na mwana-punda, mtoto wa punda.
6. Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,
7. wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake.
8. Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; na wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza njiani.
9. Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.
10. Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?