Mt. 14:32-36 Swahili Union Version (SUV)

32. Nao walipopanda chomboni, upepo ulikoma.

33. Nao waliokuwamo ndani ya chombo wakamsujudia, wakisema, Hakika wewe u Mwana wa Mungu.

34. Na walipokwisha kuvuka, walifika nchi ya Genesareti.

35. Na watu wa mahali pale walipomtambua, walituma watu kwenda nchi zile zilizo kandokando, wakamletea wote waliokuwa hawawezi;

36. nao wakamsihi waguse hata pindo la vazi lake tu; na wote waliogusa wakaponywa kabisa.

Mt. 14