Mt. 14:17-20 Swahili Union Version (SUV)

17. Wakamwambia, Hamna kitu hapa ila mikate mitano na samaki wawili.

18. Akasema, Nileteeni hapa.

19. Akawaagiza makutano waketi katika majani; akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akabariki, akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi, wanafunzi wakawapa makutano.

20. Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate, vikapu kumi na viwili, vimejaa.

Mt. 14