Mt. 14:13-15 Swahili Union Version (SUV)

13. Naye Yesu aliposikia; hayo, aliondoka huko katika chombo, akaenda mahali pasipo watu, faraghani. Na makutano waliposikia, walimfuata kwa miguu kutoka mijini mwao.

14. Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.

15. Hata kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea, wakasema, Mahali hapa ni nyika tupu, na saa imekwisha pita; uwaage makutano, waende zao vijijini, wakajinunulie vyakula.

Mt. 14