Mk. 4:11-18 Swahili Union Version (SUV)

11. Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, bali kwa wale walio nje yote hufanywa kwa mifano,

12. ili wakitazama watazame, wasione;Na wakisikia wasikie, wasielewe;Wasije wakaongoka, na kusamehewa.

13. Akawaambia, Hamjui mfano huu? Basi mifano yote mtaitambuaje?

14. Mpanzi huyo hulipanda neno.

15. Hawa ndio walio kando ya njia lipandwapo neno; nao, wakiisha kusikia, mara huja Shetani, akaliondoa lile neno lililopandwa mioyoni mwao.

16. Kadhalika na hawa ndio wapandwao penye miamba, ambao kwamba wakiisha kulisikia lile neno, mara hulipokea kwa furaha;

17. ila hawana mizizi ndani yao, bali hudumu muda mchache; kisha ikitokea dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara hujikwaa.

18. Na hawa ndio wale wapandwao penye miiba; ni watu walisikiao lile neno,

Mk. 4