Mk. 3:28-32 Swahili Union Version (SUV)

28. Amin, nawaambia, Dhambi zote watasamehewa wanadamu, na kufuru zao watakazokufuru zote;

29. bali mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hana msamaha hata milele; ila atakuwa ana dhambi ya milele,

30. kwa vile walivyosema, Ana pepo mchafu.

31. Wakaja mamaye na nduguze; wakasimama nje, wakatuma mtu kumwita.

32. Na makutano walikuwa wameketi, wakimzunguka, wakamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.

Mk. 3