Mk. 3:16-19 Swahili Union Version (SUV)

16. Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;

17. na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo;

18. na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo,

19. na Yuda Iskariote, ndiye aliyemsaliti.Kisha akaingia nyumbani.

Mk. 3