Mk. 3:12-19 Swahili Union Version (SUV)

12. Akawakataza sana, wasimdhihirishe.

13. Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea.

14. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri,

15. tena wawe na amri ya kutoa pepo.

16. Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;

17. na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo;

18. na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo,

19. na Yuda Iskariote, ndiye aliyemsaliti.Kisha akaingia nyumbani.

Mk. 3